Kikwete: Wajumbe Bunge la Katiba kutangazwa leo, kesho



Rais Jakaya Kikwete amesema uteuzi wa majina 201 ya wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba umekamilika na kati ya leo na kesho, atayatangaza pamoja na tarehe ya kuanza kwa Bunge hilo.

Bunge la Katiba litakalokuwa na wajumbe 640, litakutana kwa siku 90 kujadili Rasimu ya Katiba iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Desemba 30, mwaka jana.

“Bunge la Katiba litakutana katika wiki ya tatu ya mwezi huu. Mambo yanayosubiriwa ni mawili tu, uteuzi wa wajumbe 201 na siku ya kuanza kwa Bunge hili. Mambo haya yote ninayesubiriwa kuyakamilisha ni mimi tu,” alisema Rais Kikwete alipokuwa akihutubia katika kilele cha maadhimisho ya miaka 37 ya kuzaliwa kwa CCM.

Alisema kazi ya uteuzi wa wajumbe hao ilikamilika tangu juzi na kinachofanyika sasa ni kuhariri majina hayo na kurekebisha mambo kadhaa.

“Jumatatu (leo) tutayapitia majina haya ili tuone kama tunaweza kurekebisha. Baada ya hapo tutaweza kutangaza na inaweza kuwa siku hiyohiyo au kesho yake (Jumanne), hazitazidi siku hizi mbili,” alisema.
Alisema hivi sasa ukarabati katika Ukumbi wa Bunge, Dodoma bado unaendelea na mkandarasi ameeleza kwamba hadi Februari 10, mwaka huu atakuwa amemaliza kazi.

CHANZO: Mwananchi

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga