Simba, Mbeya City zavunja rekodi



PAMBANO la Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), kati ya wenyeji Mbeya City na Wekundu wa Msimbazi, Simba lililopigwa juzi Uwanja wa Sokoine, limevunja rekodi ya mapato baada ya kuingiza sh milioni 105.
Katika mchezo huo uliomalizika kwa sare ya bao 1-1, na kujaza melfu ya mashabiki, tiketi 21,000 ziliuzwa na baada ya makato, kila timu iliondoka na sh 25,316,630.58.

Kwa mujibu wa msimamizi wa Kituo cha Mbeya, Lwitiko Mwamundela, mgawanyo mwingine ni VAT sh 16,016,949.15, gharama za uwanja sh 12,872,702.57, gharama za mchezo sh 7,723,621.52 na Bodi ya Ligi sh 7,723,621.52.

Mgawo mwingine ni Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) sh 3,861,810.75 na Chama cha Soka Mkoa wa Mbeya (MREFA) sh 3,0003,630.58.

Msimamizi huyo aliongeza kuwa mapato hayo yamevunja rekodi ya mchezo wa mazunguko wa kwanza kati ya Mbeya City na Yanga, ambao uliingiza sh milioni 100 zilizotokana na mauzo ya tiketi 20,000.

Hata hivyo, licha ya mchezo huo kuingiza kiasi hicho cha fedha, changamoto ilikuwa ni uchache wa tiketi, ambao ulisababisha mamia ya mashabiki kukaa nje ya uwanja na wengine kuparamia miti na majengo marefu yaliyo karibu na uwanja kwa lengo la kushuhudia mchezo hadi ulipofika muda wa ‘fungilia mbwa’ ndipo walipoingia.

Akizungumzia mchezo huo, Kocha Mkuu wa Mbeya City, Juma Mwambusi, alisema matokeo ya sare ya 1-1, ni moja chachu ya kujipanga kwa ajili ya mchezo unaofuata dhidi ya Coastal Union utakaopigwa Mkwawani jijini Tanga.

Kocha huyo amewatoa hofu wadau na mashabiki wa timu kuwa ana imani mchezo utakaofuata watafanya vema ili kujihakikishia mazingira mazuri na hatimaye kubeba ubingwa.

Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic, alikisifu kiwango cha Mbeya City kutokana na uwezo waliouonyesha.
Alisema mechi za mikoani zinakuwa ngumu tofauti na zinazofanyika Uwanja wa Taifa kutokana na wachezaji kuuzoea uwanja mmoja.

“Hata hivyo, timu yangu imejitahidi kwa asilimia kubwa, lengo ilikuwa ni kushinda, kutokana na kiwango walichoonyesha Mbeya City hii pointi moja inatosha kuliko kutopata kabisa, kwani tulikuwa tuna nafasi nyingi za kushinda hasa kipindi cha pili, lakini wachezaji hawajazitumia,” alisema.

CHANZO: Tanzania Daima

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga