KAZI KWENU WABUNGE: JK aweka wazi faida na changamoto za serikali tatu


Marais wetu wakifurahia jambo
Katika Hotuba yake iliyofuatiliwa na wengi katika historia ya utazamaji wa televisheni, rais Kikwete ameonyesha kutoegemea upande wowote japo alikiri kuwa na haki ya kutoa mawazo yake.


Wengi wamefurahia uthubutu wake wa kutoegemea upande wowote japo kwa mbali sana hisia zake ziliweza kudhihirika. Amesisitiza “Maridhiano” ndio itakayowapatia watanzania katiba bora.


Hata hivyo makofi yaliweza kusikika kwa wingi kila alipoweza kuelezea changamoto za muundo wa serikali tatu; kitendo kinachoashiria kwamba wanaopenda serikali mbili wapo wa kutosha japokuwa bila maridhiano hawataweza kupata ‘Absolute Majority” vivyo hivyo hata wale waumini wa serikali tatu nao watahitaji ‘Political Compromise’ 


Mtazamo wangu: 'Katiba mpya inakuja' japo kutakuwepo na ‘Turbulence and rough ride ahead’ Wabunge wote waliopo Dodoma ni watanzania wenzetu,wenye masilahi sawa na sisi, wenye uzalendo na wenye kujitambua! 

Hivyo tuwaombe waanze kazi kwa kujali masilahi ya taifa la leo na lile taifa la kesho.

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga