RT yaburuzwa mahakamani, Mtaka atuhumu serikali

Rais wa RT aliyechaguliwa kinyume cha sheria namba 12 ya BMT iliyotungwa na bunge 1967 alinukuliwa akisema “Serikali ilikata majina ya waliokwenda nje ya nchi kujiandaa na michezo ya Jumuiya ya Madola"

Laiti angejua wala asinge nena bora angepiga kimya; ‘Tangu lini serikali kwa maana ya wizara ikawa na maamuzi ya mwanariadha gani aende na yupi asiende’ RT ndiyo kiungo kati ya serikali na wachezaji.

Mwanariadha chipukizi ATSON MBUGI ambaye ni mwalimu wilayani Kilindi Tanga alijikuta akisoma jina lake kwamba yupo New Zealand wakati yeye alikuwa Kilindi akifundisha darasani.

Kocha maarufu nchini mwenye vigezo vya juu kabisa vya (IAAF) SAMWEL TUPA naye ameachwa kinyemela lakini jina lake likasomeka yupo New Zealand!

MASWALI MAZITO: Nani aliyeenda, nani alipaswa kwenda, kwa nini majina yameleta utata, kwa nini kuna usiri? Je posho zao nani kachukua?


Ni wajibu wetu kufahamu jinsi gani pesa za walipa kodi inatumika wakati kuna fungu kutoka vyama vya michezo duniani inapaswa kutumika.

Je majina yote mawili kukosewa ni bahati mbaya ama kusudi? 


Je RT baada ya kushitakiwa mahakamani kwa kudaiwa zaidi ya Tsh: 20,000,000 viongozi watata na wasiojitambua wa RT wanapaswa kuendelea kujiita viongozi waadilifu wa taasisi hiyo muhimu isiyo na katiba?

‘Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michechezo wafukuze kazi Nyambui na ndugu yake wa ukoo Anthon Mtaka hata kama ni shemeji zako”
 

RT imekuwa kichaka cha kuchota fedha hazina na kupeleka watu baki. 

Katibu wa RT anamwachia nani ofisi badala ya kumwacha kocha kwenda na timu kambini? POSHO tu ndiyo inayowazingua wa viongozi RT?

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga