Glasgow: BMT na RT wametupotezea medali zetu watanzania, wamlaghai JK

Siku ya kuagwa timu ya Tanzania ya Jumuiya ya Madola rais Jakaya Kikwete hakutaarifiwa kwamba viongozi wa RT walichaguliwa kinyume cha katiba na pia kinyume cha sheria # 12 iliyotungwa na bunge 1967.

Lakini pia waziri Bernard Membe amejikuta akitoa pesa za watanzania kwa wahuni waliodharau katiba ambayo ndiyo msingi wa kila kitu. Ningepata wasaa wa kumuuliza waziri Membe ningemuuliza kwamba 'Ni kwa nini hakusumbuka kupeleleza uhalali wa RT'?

Hata hivyo nampa pongezi hili 'Thanks BUT no thanks Hon. Membe' kwa kuwa ametoa pesa ambazo zilitumika kubagua wanamichezo sababu wanariadha waliokwenda kambi za nje HAWAKUSHINDANISHWA na wenzao ili kubaini nani bora atakayeweza kuiletea Tanzania medali.

Kwa maana nyingine waziri ameshiriki kubariki RT kubagua uwepo wa wanawake katika timu ya riadha ya taifa 'Ama kwa kujua ama bila kujua'

Kenya kwa siku ya jana tu wamekusanya medali TANO, Uganda nao wamenyakua medali lakini sisi tunamdanganya rais wetu!  

"HONGERA NYAMBUI KWA KUFANIKIWA KUMLAGHAI JK, WE MKALI UNAMDANGANYA HADI RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO"

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga