Lipumba: Tuwekeze katika michezo

Ni ndoto kwa Tanzania kufanya vizuri kwenye michezo kitaifa na kimataifa bila kuwekeza kwenye kukuza vipaji vya vijana kama ambavyo zimefanya nchi nyingine duniani.

Huo ni ushauri wa Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba katika mahojiano maalumu na gazeti hili mwishoni mwa wiki.
Prof Lipumba, ambaye mbali ya kubobea katika uchumi na siasa, alisema Tanzania haina budi kuwekeza katika michezo kuanzia elimu ya awali, msingi, sekondari hadi vyuo vikuu ambako vipaji vipya vitaweza kuibuliwa.
Alisema Tanzania imekuwa ikifanya vibaya kimichezo kutokana na watoto wake wengi kudumaa kimwili kutokana na lishe duni kwao na wazazi wao.
“Tunafanya vibaya kimichezo, tunatafuta sababu, lakini sababu zipo katikati yetu,” alieleza Prof Lipumba na kuongeza kuwa asilimia 42 ya watoto nchini wamedumaa, jambo ambalo linawaathiri katika mambo mengi yakiwamo michezo. Msomi huyo ambaye ni shabiki wa klabu ya Simba alisema uwekezaji ambao umefanywa kwa mfano na klabu ya Azam, ni mfano mzuri ambao siku za usoni utazaa matunda.
Alishauri Serikali Kuu na hata zile za mitaa nchini kufikiria namna ya kuyasaidia maeneo yote ambayo yanatoa vipaji vingi yakiwamo Singida, Arusha na Manyara na kuyasaidia katika kuandaa wanamichezo bora wa siku za usoni. “Kuna mikoa kama Singida na mingine ni maarufu kwa vipaji katika riadha, tuwekeze pia huko, tuone matokeo yake,” alieleza.
Alishauri klabu mbalimbali za michezo ikiwamo soka kuangalia mchango wa makocha wazawa ambao wakipewa nafasi wamekuwa wakifanya vizuri na kuiletea sifa nchi.

CHANZO: Mwananchi

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga