Jamali Malinzi, wadau kumlipa Kim

Jamali Malinzi
Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi jana alitangaza rasmi kuondolewa kwa kocha Kim Poulsen, lakini akashindwa kueleza sababu za kuachana na mwalimu huyo kutoka Denmark.

Malinzi, ambaye uongozi wake ulifanya kituo cha kuteua wachezaji wa timu ya taifa badala ya kazi hiyo kufanywa na kocha, pia jana aliongeza alitangaza kuwa fidia ya kuvunjwa kwa mkataba wa Poulsen zitalipwa kwa ushirikiano baina ya TFF na wadao, ambao pia hakuwataja.
Poulsen, ambaye analipwa mshahara na serikali kutokana na ahadi ya Rais Jakaya Kikwete, ana mkataba unaoisha Mei mwakani  na alipewa kazi hiyo baada ya kuonyesha mafanikio kwenye timu za vijana.
Hivyo, kuvunjwa kwa mkataba huo kutalifanya Shirikisho hilo limlipe Poulsen mishahara yake ya miezi sita kulingana na mkataba wake. “Jukumu la kulipa gharama za kuvunja mkataba zitabebwa na TFF na baadhi ya wadau wa soka watatusaidia nusu gharama,” alisema Malinzi wakati alipoongea na waandishi wa habari jana kwenye ofisi za Shirikisho. 
Alipotakiwa awataje baadhi ya wadau hao, Malinzi alisema hata yeye ni mdau na kudai kuwa wako wengine wengi. Malinzi alithibitisha kuondolewa kwa kocha huyo na kwamba TFF inaendelea na mchakato wa kutafuta mrithi wake. 
Tayari, TFF ipo kikaangoni ikilaumiwa na wadau wake kwa uamuzi wa kubeba majukumu yasiyoihusu likiwamo la kuteua wachezaji wa timu ya taifa ambayo itacheza mechi ya kirafiki na Namibia wiki ijayo.
Kitendo cha TFF kuteua wachezaji wa timu ya taifa kinaonekana kuwa kimepitwa na wakati kutokana na soka la kisasa kutaka wataalaamu ndio wateue timu na kutetea uteuzi huo.
TFF pia inalaumiwa kwa uamuzi wake wa kusitisha  matumizi ya tiketi za kielektroniki bila ya kufanya utafiti yakinifu wa matatizo ya mfumo huo.
TFF pia inalaumiwa kwa uamuzi wake wa kuchezesha mechi za kombaini ya mikoa kwa lengo la kuibua vipaji kwa ajili ya timu ya taifa itakayokuwa ikisaka tiketi ya kucheza fainali za Mataifa ya Afrika za mwaka 2015.
Kuhusu mrithi wa Poulsen, Malinzi alisema wapo katika hatua za mwisho za kumpata kocha ambaye alisema huenda atatoka  Uholanzi au Ujerumani.

CHANZO: Mwananchi

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga