Posts

Showing posts from February 16, 2014

MATOKEO: Mfumo mpya ‘ahueni’ kidato cha nne

Image
Dr Kawambwa/Waziri Elimu   Kwa matokeo kidato cha nne 2013 bonyeza hapa: Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), limetangaza Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa kidato cha nne wa 2013, huku ufaulu ukiongezeka kwa asilimia 15.17. Matokeo hayo ni ya kwanza tangu kuanza kutumika kwa mfumo mpya wa upangaji ambao ulipanua wigo wa alama na madaraja, hivyo kutoa nafasi kubwa zaidi kwa watahiniwa kufaulu. Licha ya kuanza kutumika kwa mfumo huo, idadi ya waliofeli imeendelea kuwa kubwa kwani watahiniwa 151,187 sawa na asilimia 42.91 wamepata sifuri. Kati ya hao, wavulana ni 78,950 sawa na asilimia 41.54 na wasichana ni 72,237 sawa na asilimia 44.51. Kadhalika matokeo hayo yameendelea kushuhudia baadhi ya watahiniwa wakiandika matusi kwenye karatasi zao za majibu, huku wengine wakichora vitu vya ajabu kwenye mitihani hiyo, huku wengine wakishindwa kuandika chochote kwenye karatasi hizo. Akitangaza matokeo hayo jana jijini Dar es Salaam, Kaimu Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde al

JK mgeni rasmi miaka 30 ya kumbukumbu ya kifo cha Sokoine

Image
Kutakuwa na mbio za kilomita 2 kwa watoto wa shule za msingi na sekondari, pia waheshimiwa viongozi wa serikali, viongozi na wakuu wa vikosi vya ulinzi na usalama pia watashiriki mbio za kilomita 2 kama ilivyokuwa mwaka jana.

A day in the life of the Sochi 2014 Olympic medals

Image
And the medals find their owners! The winners of the Ladies’ 500m short track event: Silver: Arianna FONTANA (ITA), Gold: LI Jianrou (CHN), and Bronze: PARK Seung-Hi (KOR). Ever wondered how the Olympic medals are stored at an Olympic Games? Who keeps an eye on them? How they’re transported to the Medals Plaza? Or what goes on backstage to ensure the medals look their shiny best before being presented to the athletes?. SOURCE: olympic.org

Wanariadha mashuhuri kuchuana Kili Marathon

Image
John Bayo/Mwingereza/Musa Ninga WANARIADHA mashuhuri wa Tanzania wanatarajiwa kupambana vilivyo ili kutwaa medali na fedha katika mbio za Kilimanjaro Marathon 2014 zinazotarajiwa kufanyika Machi 2 mjini Moshi. Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa mbio hizo, John Bayo, wanariadha maarufu wa Tanzania, Andrew Sambu, John Leonard na Daudi Joseph ni miongoni mwa wanariadha Watanzania watakaoshiriki katika mbio za Km 42 kwa wanaume. Katika mbio za kilomita 42 kwa wanawake, watakuwepo Banuelia Brighton, Fabiola William na Flora Yuda, ambao wanatarajiwa kutoa upinzani mkali kwa wanariadha wengine Watanzania pamoja na wa kigeni. Andrew Sambu ana rekodi ya kumaliza Korea Marathon kwa saa 2:09:52 mwaka 2004 na mshindi wa medali ya fedha kwenye Mashindano ya Riadha barani Afrika na ameshiriki Olimpiki, wakati Banuelia Brighton akiwa ameshinda Kigali Peace Marathon mwaka 2009 na kumaliza wa pili Kampala Marathon mwaka 2011. Dickson Marwa, mshindi wa Ngorongoro Half Marathon 2013 ambako