BARUA YA WAZI KUTOKA KWA MWANARIADHA WA ZAMANI WA TANZANIA




Wazee,

Nakumbuka sana wakati nilikuwa nasoma Kibasila Secondary School pale Chang'ombe karibu na uwanja wa chuma yaani uwanja wa taifa, kila mara nikitoka shuleni nilikuwa napita pale uwanjani ili nikawaone wanariadha wa timu ya JWTZ na JKT wakifanya mazoezi ya uwanjani.

Nawakumbuka wakina Gwangwai, Kijuu, Ndemandio, Francis John na wengineo ambao walikuwa wakifanya mazoezi ya mbio za mita 10,000, walikuwa wakipiga mita 400x20 wanapunzika kwa kujogi mita 200 na walikuwa wakizipiga sekunde 60 kila moja na mbili za mwisho walikuwa wakizipiga kwa sekunde 56.

Upande mwingine walikuwa Musa Luliga, Kijuu na Marwa kwa jina jingine Alberto Juantorena wanapiga mita 300x15 walikuwa wanazipiga kwa sekunde 36 na ya mwisho wanaileta kwa sekunde 34.
Hawa jamaa zetu walikuwa hawapati mialiko tuu, wao walikuwa wanasubiri michezo ya majeshi, nina hakika kama wangepewa nafasi ya kwenda Oslo, Berlin au Stockholm Grand Prix wangefanya maajabu kabisa.

Jamani tuwakumbuke hawa ndugu zetu kwa kuwa wanamichezo wenye viwango vya juu sana, Pia mavazi yao yalikuwa makuchi kuchi ya kampuni Ya UMBRO na raba za Bata wakati huo au yale mabuti laini ya jeshi kutoka jeshi la China wakati huo.

Wakati wa mashindano ya taifa ikipigwa mita 10,000 waliokuwa wakiita mbele walikuwa Gwangwai, Francis, Ndemandoi na wengineo kutoka JWTZ tuu. Mita 1500 alikuwa Kijuu, na mita 800 alikuwa Alberto Juantorena.
Kwenda kukimbia Zanzibar ilikuwa starehe tuu, maana uwanja wao ulikuwa wa kisasa.

Je, RT ina mpango gani ya kuwaalika wakimbiaji wetu wa zamani ambao bado wako hai kwenda kwenye mashindano ya taifa mwaka huu?, Ni muhimu tukumbuke na pia RT ingeanzisha chumba au sehemu ya kumbukumbu ya wachezaji hawa muhimu kwa taifa.

Kuna wachezaji wengi tuu ambao wameitangaza nchi yetu, nitata wachache lani kama kuna mtu anawafahamu wengine ongeka majina kwenye orodha;

Agapius Masong, Mohamed Rutiginga, Kijuu, Francis John, Gwangwai, The Shahanga brothers, Alphonce Swai, Timothy Kamili, John Haigaimo, Petro Meta, Mrashani, Simon Peter, The Naali brothers, Sambu, Umbe, John Yuda na wengine wengi tuu ambao wamesahaulika.

Kuna umuhimu ya kufufua mchezo huu mpendwa wa riadha maana wengine ndio unatupa chakula mpaka leo.

Nitaendelea siku nyingine,


Jimmy.

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga