MTAZAMO: USHINDI WA URAIS TFF UNAKWENDA KWA JAMALI MALINZI



Jamali Malinzi

Baada ya mvutano wa muda mrefu baina ya TFF na ‘Hali Halisi’ yaani katiba ya haki sasa uchaguzi utafanyika October 27, 2013, hiyo ni baada ya wenye masilahi binafsi kushindwa kumzuia Jamali Malinzi kugombea ‘sasa wana haha’


Mtazamo wa sasa ni kwamba wajumbe na wadau wengi wa soka nchini wamechoshwa na ujanja ujanja mwingi uliozoeleka, mara nyingi waliopo madarakani hutumia nguvu yao ya kiofisi (Abuse of Power) kuwabana wanaowania madaraka kwa kulinda masiliahi yao waliyojichotea wakati wakiwa madarakani.


Hata kama wao wenyewe hawagombei lakini watawapandikiza vibaraka (Puppets) ambao watalinda ule mnyororo wa kifisadi ndani ya ofisi hizo.


Shaffih Dauda amejikuta akiporwa fedha zilizodaiwa kuwa faini na kamati iliyojiita (chombo cha juu cha maamuzi); cha kushangaza ni kwamba chombo cha chini kilipobatilisha maamuzi, chombo hicho cha juu hakijalalamika. ‘Kitendo kinachoashiria kuwa ni Syndicated Matter’ hivyo Shaffih akatolewa kafara.


Je wanaojitahidi kuharibu michezo Tanzania wataendelea hadi lini? Bila shaka wapiga kura wa uchaguzi mkuu wa TFF ndio wenye dhamana ya kuweka NUKTA ya ujanja ujanja huo kwa kuwachagua viongzi wenye kujali “UTAIFA KWANZA”.

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga