Spoti Kizaazaa hewani TBC: Kituo chako cha televisheni ya Taifa

Ally Hozza ni miongoni mwa watoa hoja
Ndugu wapendwa kile kipindi kinachopendwa na watanzania wengi kutokana na kuwa mstari wa mbele kutoa ukweli kuhusu kudorora kwa michezo nchini kinarudi hewani.

Spoti Kizaazaa kinarudi kwa kishindo kupitia Televisheni ya Taifa (TBC), kituo kinachobeba kauli mbiu ya "Ukweli na Uhakika". Kitakuwa kinarushwa kila Jumapili saa TATU UNUSU usiku.

Awali Spoti Kizaazaa kilikuwa kikirushwa na ITV, hadi mkataba wa muda ulipoisha ndipo kikakwama kwa muda wakati mpango mwingine mzuri zaidi ukisukwa na waandaaji wa kipindi hicho maarufu sana.

Awali mjumbe moja wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (Peter Mwita) alinukuliwa na "Private Investigator" akidai kwamba "Fedha nyingi za TOC ndio zimezima vuguvugu la Spoti Kizaazaa lililojaa genge la wahuni". 

Kauli hiyo haikuwafurahisha wengi lakini sasa furaha imerudi na nukuu hizo zenye thamani ya bia mbili hazitunyimi wanaharakati wa michezo usingizi.

Wote mnakaribishwa kushiriki kutoa maoni yenu na pia kusikiliza maoni ya wadau wenzako.


Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga