YOHANA MWILA: MWANAMICHEZO MLEMAVU WA TANZANIA ALIYE HUJUMIWA AFRIKA KUSINI

Yohana Mwila
Hivi karibuni Tanzania iliwakilishwa na wachezaji watatu walemavu katika mashindano tennis ya Airport Company yaliyofanyika katika mji wa Port Elizabeth Afrika Kusini. 

Wachezaji hao walemavu waliowakilisha nchi yao ni pamoja na Novatus Temba, Yohana Mwila na Juma Hamisi ambao wote ni wachezaji wa tenisi, mara nyingi hawakosekani katika viwanja vya Gymkhana Dar Es Salaam. 
Wachezaji hao mahiri walifuatana na mwalimu wao (coach) Riziki Salum ambaye kazi yake kubwa ni kuwaongoza na kuhakikisha kwamba wachezaji wake wanasafiri na kufika salama, wanapata malazi na chakula na pia kuhakikisha kwamba wanashiriki mashindano na kupewa matokeo halali. 
Hata hivyo uchunguzi umebaini kwamba mwalimu huyo hakufanya kazi yake kizalendo kwani safari aliyotumwa aliibadili na kuwa safari yake ya kutalii. 
Uchunguzi umeonyesha wazi kwamba vipindi vyote ambavyo wachezaji walipambana kuiletea sifa Tanzania kocha huyo hakuwepo uwanjani kushuhudia na kutetea matokeo ya watanzania aliotumwa kuwatetea. 
Matokeo ya uzembe wa mwalimu huyo umeisababishia nchi (Tanzania) hasara ya kukosa ushindi kutokana na mchezaji Yohana Mwila kubadilishiwa matokeo ambayo alipambana hadi kufikia hatua ya robo fainali. 
Yohana Mwila alitegemea kucheza nusu fainali katika mchezo wa singles, hivyo akaendeleza mapambano katika mchezo wa doubles
Wakati yeye anacheza katika doubles makocha wa Afrika Kusini wakapanga njama ya kubadili matokeo na nusu fainali ikaendelea katika uwanja wa pili huku Yohana akipambana katika uwanja mwingine. 
Lakini ghafla wakati wa chakula cha jioni Mwila alibaini kwamba fainali za singles zimesha chezwa!, mara moja akatoa malalamiko kwa wahusika. 
"Niliambia ni kweli kuna kosa limefanyika, na kwamba watarekebisha kesho ila niliambiwa kocha wako yupo wapi?, ndiye anayestahili kutetea haki zako" alisema Mwila kwa huzunu kabisa. 
Hivyo hapana shaka kwamba kosa lilifanyika, lakini hata kesho yake kocha Riziki Salum hakuonyesha bidii zozote na hatimaye hakijarekebishwa kitu!. Badala yake bwana Riziki alikazania kwamba "sasa hatuna la kufanya, labda tuwaombe wahusika watupendelee kwa siku zijazo" alinukuliwa akisema mwalimu huyo asiye mzalendo hata tone. 
Viongozi wa Paralympic mpo wapi?, au mnapenda kuwaonea vilema wenzenu wakionewa?, ili hali mungu amewapa ninyi ulemavu, na mnafahamu uchungu wa kuwa walemavu lakini bado mnabariki uonevu wanaofanyiwa walemavu kwa kuto sema chochote!. 
Kama hiyo haitoshi rais na katibu wa Paralympic (Johnson Jason Meela na Iddi Kibwana) bila kujali wala kuheshimu katiba wamekaidi utaratibu wa kufanya uchaguzi uliopaswa kufanyika 2010 ili waendelee kukaa madarakani, kitendo ambacho ni cha uonevu dhidi ya wachezaji walemavu. 
Waswahili wanasema "kila mtu ana myonge wake" bila shaka wachezaji walemavu waliopo chini ya chama cha Paralympic ni wanyonge wa viongozi wa Paralympic; japo kuwa ni wasomi sana na hata wengine ni wanasheria.

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga