MAJANGA: Marekebisho ya katiba ya RT haitambui masilahi wala uwepo wa muungano kwa kuitenga Zanzibar


ZANZIBAR TANZANIA
Augosti 25/2013 Chama Cha Riadha Tanzania (RT) kilijipanga kupitisha rasimu ya katiba ya chama hicho Morogoro kabla ya kuwashirikisha wadau na wanariadha waliopo mikoani.

Kwa bahati nzuri BMT waligundua tatizo na kutoa tamko la zoezi hilo kuahirishwa hadi hapo wadau mbali mbali nchini watakaposhiriki kutoa maoni ya vipengele vya katiba hiyo.

Pamoja na zoezi hilo kutofanyika ipasavyo hadi sasa Zanzibar imestuka na kupinga kutoshirikishwa kwake hata katika TAFSIRI ya katiba hiyo, kitendo ambacho kimesababisha wazanzibari kuamka na kutaka ufafanuzi kutoka kwa viongozi wa RT.

Zanzibar hatutambuliwi na shirikisho la riadha duniani (International Association of Athletics Federation) halafu eti tusitambuliwe pia na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania” alihoji mdau muhimu wa riadha kisiwani Zanzibar.

“Pia sisi wadau wa Zanzibar tunataka mgao wa fedha zinazotokana na IAAF kwani sisi ni nchi mbili zenye mahitaji sawa maana sisi ni muunganiko wa vitu viwili vilivyopo sawa” mdau mwingine aliongezea.

Madai ya wazanzibari yanachukua uzito wenye mashiko sababu nchi yetu hivi sasa ipo katika mpito wa kihistoria kwa kipindi hiki cha kuandaa katiba mpya yenye makusudi ya kuimarisha muungano wetu; hivyo haileti maana yoyote pale ambapo vyama vya michezo vinaleta chembe chembe za utengano.

Ni muda muafaka sasa viongozi wa BMT na BMZ kukaa na kuangalia namna bora ya kutatua hitilafu hii isiyoonekana kwa viongozi wasioheshimu hata katiba zao wala kuona mbele.

Bila shaka M/Kiti wa BMT Deoniz Malinzi ataona umuhimu wa kuhifadhi fedha zake alizoahidi kuzitoa kwa kugharimia zoezi hilo la kupitisha katiba November 30/2013 Morogoro hadi hitilafu hizo za KERO ZA MUUNGANO michezoni zitakapowekwa sawa.

Vinginevyo posho za mikutano zitatafunwa hatimaye katiba kukwama na Tanzania ikaendelea kupata aibu kwa gharama ya siasa chafu viwanjani.


Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga