Mataifa 21 kushiriki Uhuru Maratho

Innocent Melleck/Katibu wa Kamati ya Uhuru Marathon


WANARIADHA kutoka nchi 21 wanatarajiwa kushiriki mbio za Uhuru Marathon zinazotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam Desemba 8, mwaka huu.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa Kamati ya Uhuru Marathon, Innocent Melleck, alisema kujitokeza kwa wanariadha kutoka mataifa mbalimbali kumeongeza hamasa kubwa ya mbio hizo.
Melleck alisema wanariadha kutoka mataifa hayo ndio wamejiandikisha hadi sasa na wanaamini wengi wataendelea kujitokeza ili kufanikisha lengo lake.
Alizitaja nchi wanazotoka wanariadha hao hadi sasa kuwa ni Tanzania, Uganda, Kenya, Afrika Kusini, Ethiopia, Angola, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Malawi, Marekani, Ujerumani, Jamaica, Urusi, China, Japan, Venezuela, Comoro, Nigeria, Italia, Canada, Madagascar na Uturuki.
“Hii ni faraja kubwa kwetu, kwani inaonyesha kwa kiwango kikubwa lengo letu la kupigania amani, umoja na mshikamano miongoni mwetu linakubalika na watu wengi duniani,” alisema.
Aidha, Melleck alisema usajili bado unaendelea kwa wale wanaotaka kushiriki, ambako fomu zitakazotolewa kwa mshiriki wa kilomita 3 atalipa sh 100,000, kilomita 5 sh 2,000 na washiriki wa kilomita 21 na 42 watalipia sh 6,000.
“Tunachukua nafasi hii pia kuziomba kampuni au taasisi mbalimbali zinazotaka kudhamini mbio hizo zijitokeze na kufanya hivyo, kwani nafasi bado ipo na tukumbuke bila amani hakuna chochote kinachoweza kufanyika,” alisema.
SOURCE: Tanzania Daima

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga