Mkutano wa Katiba RT waota mbawa

Suleiman Nyambui/Katibu RT

MKUTANO mkuu wa kupitisha rasimu ya Katiba ya Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), uliokuwa ufanyike mjini Morogoro Novemba 30 umepigwa kalenda.

Akizungumza na Tanzania Daima jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa RT, Suleiman Nyambui, alisema mkutano huo umeahirishwa hadi utakapotangazwa tena baada ya kuingiliana na sherehe za ujio wa Kombe la Dunia litakalowasili nchini Novemba 29.

Alisema tayari ameanza kuwatumia taarifa wajumbe mbalimbali wa mkutano huo kupitia njia ya barua na mtandao ili kuhakikisha taarifa hizo zinawafikia kwa wakati na kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza kwao.

“Viongozi wote watakuwepo katika sherehe hizo, hivyo kamati ya utendaji imeona isogeze mbele mkutano ili kuwapa nafasi wajumbe wetu kulishuhudia kombe hilo, na ninaamini taarifa zitamfikia kila mmoja na hakutakuwa na tatizo lolote,” alisema Nyambui.

Kutokana na hali hiyo, aliwataka wajumbe wa mkutano huo kuwa wavumilivu na kujiandaa kwa ajili ya mkutano huo hadi itakapotangazwa tena siku utakapofanyika.

Lakini wakati Nyambui akitoa taarifa hizo, baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Utendaji na viongozi wa vyama vya mikoa, wameelezea kukerwa na kitendo hicho, kwani tayari walikwishaomba ruhusa kwa waajiri wao, na RT imechelewa kutoa taarifa rasmi ya kuahirishwa.

“Kama wamekosa fedha wangetuambia tu mapema, lakini mara tunasikia fununu kuwa tatizo sio fedha bali ziara ya Kombe la Dunia, hivi kweli hivi vitu vinaingiliana kweli?” alihoji kiongozi mmoja kutoka Tabora.

SOURCE: Tanzania Daima


Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga