Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni: Kesho ni mbio za Karatu Sports Festival



Mbio za Karatu Sports Festival kesho zinapigwa mjini Karatu mkoani Arusha kwa hisani ya Kamati ya Olimpiki Tanzania ikiwa ni tawi dogo la Kamati ya Olimpiki ya Dunia.

Kwa vile ni haki kujali jitihada zozote zinazofanywa na wadau wa michezo sina budi kuwakumbusha waandaaji mbumbumbu wanaotimukia kuandaa ‘gemu zisizo zao’ wajifunze angalau jambo moja ama ama zaidi ya moja katika mbio za kesho.

Kwamba si lazima uwaalike wakenya ama mataifa ya mbali ili kuwadanganya wadhamini wakukubalie! Ikumbukwe kuwa sababu kubwa ya kuandaa mashindani ni kuhamasisha watanzania na kuwawezesha ili kuibua vipaji vipya.

Hivyo siyo haki kutangazia umma kwamba Gebresselassie na Kiplagat wanakuja kumbe uongo mtupu! ‘UHURU MARATHON WALITUMIA VYOMBO VYA HABARI KUPOTOSHA UMMA MAKUSUDI’ 

Pamoja na mengineyo utapeli uliofanyika kwa kumnyima zawadi mshindi wa NNE mtanzania wa Mbulu (ALEX SANKA) na kumpa mkenya zawadi hiyo, hadi leo mtanzania huyo anateseka kudai fedha alizozishinda kwa nguvu na jasho lake mwenyewe bila kupata maji ya kunywa njia nzima ya kilomita 42.

Pamoja na hayo kifo kilichosemwa kunyamazishwa bila tamko lolote rasmi la kukanusha ama kuthibitisha. Athletics Kenya pia walikanusha kutoa kibali hata kimoja kwa wanariadha wake waliodaiwa kuwa na vibali halali. Denis Malley na mwaandaaji wa Uhuru marathon aibu yao, UCHUNGUZI LAZIMA.

Nawapongeza waandaaji wa Karatu Sports Festival kwa kujali Utaifa Kwanza kwa shughuli hiyo ya kesho, ninashauri kwamba mbio hizo zifanyike kwa mzunguko katika mikoa mbalimbali badala ya kufanyika Karatu kila mwaka ili hamasa ya mbio hizo zienee nchi nzima.  

'TANZANIA HAIPO KARATU BALI KARATU NDIYO IPO TANZANIA; TUIPENDE TANZANIA YOTE BILA KUBAGUA KAMA RAMANI YETU ILIVYO'

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga