SAMBU: Mkongwe wa riadha Tanzania afanikiwa kufikia kiwango cha kuwakilisha Tanzania katika Marathon Jumuia za Madola Glasgow 2014

Andrea Sambu (Left)

 Mwanariadha mkongwe nchini amefanikiwa kuingia ndani ya Qualification Standard ya kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Jumuia ya Madola yanayotarajiwa kufanyika mwakani mjini Glasgow Scotland.

Sambu alikimbia masaa 2:14:30 katika mashindano ya Donzhou Interanational Marathon nchini China December 21, 2013 kwa kumaliza akiwa nafasi ya tisa (9) na kufanikiwa kuingia ndani ya kumi bora.
Andrea Sambu mwenye umri wa miaka 41 ndiye mwanariadha pekee mtanzania aliyewahi kutwaa ubingwa wa dunia katika mbio za nyika (World Cross Country Championships) miaka 22 iliyopia (1991).
Bila shaka chama cha riadha RT kitamwandalia mazingira mazuri Andrea Sambu kwani hadi sasa yeye na Musanduki Mohamed pekee ndio waliokimbia muda unaokubalika katika mashindano ya jumuia za madola katika nchi nzima.
 “Ninafurahi kwamba nimekuwa katika ngazi ya kimataifa kwa zaidi ya miaka 25 hadi sasa, nashindana na vijana wadogo ambao wengine wana umri sawa ama chini ya umri wa watoto wangu” Sambu alisema akiwa na furaha.
“Ningweza kushinda mbio za juzi ila nililazimika kukaa Airpor ya KIA kwa siku nzima kutokana na ndege ya Ethiopia kutua Arusha kwa dharura, hivyo nilisafiri kwa shida na kufika China saa 10 alfajiri na kuunganisha mashindano saa moja asubuhi bila kulala na uchovu wa flight ya zaidi ya masaa 15” Sambu aliendelea kuelezea.

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga