Wilbard Peter na Catherine Lange watwaa ubingwa Karatu Sports Festival


Catherine Lange @ Sokoine Marathon

Leo mji mdogo wa Karatu uliopo jirani kabisa na Ngorongoro Crater umeshuhudia mbio za kasi za umbali wa kilomita 10 zilizoshirikisha wanariadha wa Tanzania.
Wilbard Peter wa Chuo cha Polisi Moshi (CCP) alishika nafasi ya kwanza akifuatiwa na John Leonard wa Hakika Club na nafasi ya tatu kuchukuliwa na Joseph Theophil wa Guang Club ya Mbulu.
Kwa upande wa wanawake mwanariadha mahiri Catherine Lange wa timu ya Magereza Arusha alishinda, nafasi ya pili ikidhibitiwa na Merry Naali wa Ambassador Club na nafasi ya tatu ikienda kwa Angelina Tsere waWSSS.
Mtazamo: Kwa mtazamo wa haraka ni kwamba mbio hizo zimefana kuliko mbio zilizokimbiwa hivi karibuni kwa kujali zaidi ushiriki wa wanariadha wazalendo kwa kutozingatia ushiriki wa wanariadha kutoka nje ya Tanzania.
Usumbufu unaojitokeza mara nyingi ni pale ambapo MAWAKALA wa wakimbiaji wa nje ya nchi huwa wanafanya UHUNI wa kuwadhulumu wakimbiaji wazalendo kwa kuwapendelea zaidi wakenya ili wao MAWAKALA wajipatie ASILIMIA ndani ya Price Money ya wageni.
Sokoine Mini Marathon pia ilikuwa mbio iliyofana sana kwa kujali wanariadha wazalendo zaidi ili zawadi wanazopata ziweze kusitiri maendeleo yao hatimaye waweze kuwakilisha nchi yao vyema hapo baadaye.

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga