Georgina na Mallya waongoza vyema ‘Team Tanzania’ kuelekea ushindi wa jumla wa mashindano ya East African Junior Tennis Championships


Emmanuel Mallya
Vijana chipukizi wa Tanzania Georgina Kaindoah, Emmanuel Mallya na wenzao  wamefanikiwa kuingia roundi ya pili ya mashindano ya tenisi ya vijana wa umri chini ya miaka 16.

Mashindano hayo yanayofanyika katika viwanja vya Gymkhana mjini Dar Es Salaam yalifunguliwa rasmi juzi na afisa mwandamizi wa wa International Tennis Federation ukanda wa Africa Mashariki ndugu Thiery Ntwari.


Hadi sasa timu machachari ya watoto mahiri wa kitanzania inaongoza kwa uwingi wa waliovuka roundi ya kwanza. 

Kwa upande wa vijana wanaume (under 16 yrs) Sadik Ibrahim amemshinda Mollazewdu Nehemia wa Ethiopia, Menard Frank akimbwaga Kigotho Olivier wa Kenya na Emannuel Mallya akifanikiwa kumshinda Hassane Maulida wa Comoros. 


Wasichana under (16 yrs) Georgina Kaindoah alimshinda Zeru Maldhere wa Ethiopia na anatarajiwa kucheza tena leo na Nkata Judy wa Kenya. 

Kwa mtiririko huu wavulana wote wa Tanzania wamefaniukiwa kuingia robo fainali huku msichana Georgina Kaindoah amefanikiwa kuingia nusu fainali.


Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga