BUNGE LA MICHEZO: "RIADHA HARD TALK 2014 MOSHI FEBRUARY 9 2014"


Domician Genandi
Watanzania wameamua kuuvaa ukweli: Holili Youth Athletic Club iliyopo mkoani Kilimanjaro inaandaa mdahalo utakaowashirikisha wanariadha wote, wadau na viongozi wa chama cha riadha.

Mkurugenzi wa Holili Youth Athletic Club ndugu Domician Rwezaura Genandi ameileza gidabuday.blogspot.com kwamba ameamua kufanya hivyo ili kutafuta kwa pamoja jinsi ya kulipatia jawabu kiu ya medali ambayo Tanzania inayo kwa muda mrefu.

“Ninaimani kwamba wote kwa pamoja tukiongea ukweli, kukosoana na kuelezana ukweli tutapata jawabu mwisho wa mazungumzo ambayo yatratibiwa kwa uwazi na ukweli” alisema mkuu huyo wa HYAC.

"Ikiwa Kweli tunapenda mchezo huu wa riadha; haijalishi wewe ni kiongozi, mdau au mwanariadha basi mdahalo huu utaupenda maana sisi HYAC tumeamua kugharimia ukumbi, chakula cha mchana wa siku hiyo na kuwapata waandishi na vyombo vyao vya habari” aliendelea kusema Domician.

Utaifa Kwanza blog inawapongeza HYAC kwa wazo hili zuri ambalo RT ingewachukua miaka Milioni kupata idea hiyo na kwamba ‘TUPO PAMOJA’ Siku hiyo 'Moshi itatoa Moshi mweupe kama alama ya ushindi wa kimawazo; solution ya kuleta medali katika siku zijazo'.

Wanariadha wote mnaalikwa kusema kero zenu ili vyombo vya habari viweze kupaiza sauti zenu wakuu wa nchi wapate kusikia na kufanyia kazi mawazo yetu ya pamoja.


Comments

  1. safi sana kaka Wilhelm endelea kutuabarisha na harakati za kufikisha riadha mbele daima.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga