Andrea Sambu na Mohamed Msenduki wafuzu madola upande wa riadha


Mohamed Msenduki
Wanariadha Andrew Sembu na Mohamed Msenduki  wamefikia viwango vya kushiriki michezo ya Jumuiya ya  Madola vilivyowekwa na Shirikisho la riadha Tanzania  (AT).

   Riadha ni miongoni mwa michezo minane ya Tanzania  iliyotajwa na Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC)  kuiwakilisha nchi kwenye michezo ya madola itakayofanyika  katikati ya mwaka huu nchini Scotland. Sambu alifikia viwango hivyo kwenye mbio za Dazuo  Marathon zilizofanyika mwishoni mwa mwezi uliopita nchini  China baada ya kutumia saa 2:14:30 kwenye marathoni (km  42).

Msenduki ametumia saa 2:12:08 kwenye mbio  nyingine za marathon zilizofanyika nchini humo.
“Hatuwezi kuwaacha kwani wametumia muda mzuri ambao  RT tuliuweka kwa ajili ya wakimbiaji wetu wa madola,”  alisema Katibu Mkuu wa RT, Suleiman Nyambui. Nyambui alisema mbali na Sambu na Msenduki pia  wakimbiza upepo, Samson Ramadhan na Osward Leverian  wanajiandaa kwenda Bamaco, Mali kwenye mashindano na  wakifikia viwango watajumuishwa kwenye kikosi cha madola.

“Kamati ya ufundi ya RT iliweka muda wa kufuzu ambapo  tuliamua kutumia muda aliotumia mtu aliyekamata nafasi ya  tano kwenye michezo ya madola ya 2010 nchini India,”  alisema Nyambui.

Alisema muda huo ni saa 2:12 hadi 14 kwenye marathoni  muda ambao Msenduki na Sambu wameufikia.
Akizungumzia kambi ya timu ya taifa kujiandaa na michezo  hiyo, Nyambui alisema kinachowakwamisha kuanza ni  ukosefu wa fedha.

Awali kambi hiyo ilikuwa ianze Desemba Mosi mwaka jana  huko Hombolo na tayari RT iliwaita wanariadha 40 kwa ajili  ya kambi hiyo licha ya kuahirishwa mara kadhaa.

“Programu zimekamilika japo tunakwamishwa na ukata,  tukifanikiwa kupata fedha vijana wataingia kambini japo  hayo yatakuwa matunda ya baadaye,” alisema Nyambui. Tanzania imekuwa na rekodi mbaya kwenye mashindano ya kimataifa kwa zaidi ya miaka 10 sasa.

CHANZO: Mwananchi

NYONGEZA: Andrea Sambu alifuzu baada ya sisi wenyewe (Siyo RT) kufanya bidii zetu kumpatia Sambu mbio nchini China ndipo alipoweza kupata kiwango hicho.

Watanzania wafahamu hilo ‘kwamba RT kwa sasa ni jina la mwendawazimu! Anthony Mtaka anajenga CV aende kugombea ubunge sababu haridhiki na kazi ya DC aliyopewa na Rais Kikwete

Naye Nyambui ‘Hajitambui’ kwa kuweka kinywani kila senti anayokumbana nayo bila kujali masilahi ya nchi wala ya wanariadha! ‘Nyambui is a dead man walking’.

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga