MABADILIKO: Sokoine Marathon itakuwa kilomita 10 badala ya kilomita 21

Tunaomba radhi kwa kufanya mabadiliko ya ghafla! Hiyo ni kutokana na mashauriano kati yetu sisi waandaaji, Chama Cha Riadha Mkoa  na wanariadha wenyewe.

SABABU KUU: Imeamuliwa kwamba siyo vizuri kuwakimbiza wanariadha mbio ndefu mara mbili kwa wiki moja sababu pia kutakuwa na Ngorongoro Half Marathon April 19, 2014.

Familia imeridhia ombi letu na pia imekuwa wazo zuri kwa wanariadha wazoefu ambao wanafahamu athari za kukimbia mbio ndefu mfululizo. Pia wananchi wengi sasa wataweza kushiriki Kilomita 10.


Taratibu zingine hadi sasa zipo kama ilivyopangwa, ila namba zinasajiliwa katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid Karume. Tsh: 2,000 tu kwa kusajili namba yako. ZAWADI ZITATOLEWA KWA WASHINDI.

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga