Ikangaa, Shahanga waishangaa RT

Kanali Mstaafu Juma Ikangaa
Bingwa wa Afrika wa 1982, Juma Ikangaa na mshindi wa medali fedha ya Jumuiya ya madola, Gidamis Shahanga wamelishangaa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) kushindwa kupeleka timu kwenye Mashindano ya Afrika yanayoendelea nchini Morocco.
Wanariadha hao wakongwe wamesema kuwa, kati ya vioja vinavyofanywa na RT ni kushindwa kupeleka timu kwenye mashindano makubwa kama hayo na kusisitiza kuwa kutokwenda kwenye mashindano hayo kutaiweka Tanzania katika mazingira magumu  kwenye Michezo ya Afrika (All African Games) mwakani.
Gidamis Shahanga
Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti jana, walisema, Tanzania ilipaswa kutumia mashindano ya Afrika kuwapima wanariadha wake kwa maandalizi ya Michezo ya Afrika.
“RT imekosea kutopeleka timu Morocco, tunaambiwa imepeleka wanariadha wawili ambao  wamekwenda kuiwakilisha Zanzibar na si Tanzania bara,” alisema Ikangaa aliyewahi kuwa bingwa wa marathoni kwenye mashindano hayo ya 1982, nchini Misri.

Wakati Shahanga alisema kuna wanariadha walioonyesha uwezo mkubwa kwenye mashindano ya taifa, wameshindwa vipi kuwapeleka kushindana huko? Yale ndiyo mashindano ya kuwajenga wanariadha kabla hata ya Michezo ya Afrika, Olimpiki, Madola na hata mashindano ya dunia.
Katibu Mkuu wa RT, Suleiman Nyambui alisema Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imewagharimia wanariadha, Ally Seif na Mohamed Ibrahim waliopo Marrakech kwenye michuano hiyo ambapo wanaiwakilisha Tanzania siyo Zanzibar pekee.
“Tanzania bara hatujapeleka mchezaji kutokana na sababu  zisizozulika, hata hivyo waliopo huko wametoka Zanzibar na wamegharimiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambao wanachuana  kwenye mchezo wa kurusha kisahani, tufe na mkuki.”

CHANZO: Mwananchi

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga