Uzembe waitoa Tanzania michezo ya Olimpiki 2016

Tanzania haitashiriki michezo ya soka  kimataifa hadi mwaka 2016 kutokana na timu yake ya  vijana  wa umri chini ya miaka 23  kutoshiriki michuano ya kusaka  tiketi ya kushiriki Olimpiki  msimu wa 2015/2016.

Kukosekana kwa timu hiyo ya U-23 kunaweza kuwa uzembe  wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Katika ratiba iliyotolewa juzi na Shirikisho la Soka  Afrika (CAF), pazia la michuano hiyo litafunguliwa Desemba.
Katika michuano hiyo, raundi ya kwanza  Rwanda itaanza kukata utepe kwa kumenyana na Somalia wakati Kenya itacheza na Zambia au Botswana. Kikosi hicho mara ya mwisho kilishiriki michezo ya  Afrika mwaka 2011,  kikiwa chini ya Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ na kiliondolewa mapema kwenye michuano hiyo na Nigeria. 
Hata hivyo, U-23 haitashiriki michuano hiyo kwa vile Tanzania haikuthibitisha ushiriki wake huku viongozi wa juu wa TFF wakikwepa kulizungumzia  suala hilo.
Alipoulizwa juu ya suala hilo Rais wa TFF, Jamal Malinzi alisema kwa kifupi :”Sina taarifa nipe muda nifuatilie.” Kwa upande wake, Julio akizungumzia suala hilo alishutumu TFF kwa uzembe kwa kushindwa kufatilia wakati Tanzania mara ya  mwisho ilifanya vizuri ingawa ilitolewa hatua za mwisho. 
“Kilichopo ni uzembe tu wa wahusika wameshindwa kufuatilia.” Timu hiyo ya U23  ndiyo chimbuko la kina Shomari Kapombe, Mbwana Samata, Thomas Ulimwengu na nyota wengine.

CHANZO: Mwananchi

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga