Zitto azitaka fainali za Afrika 2017

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ameishauri Serikali isiache nafasi adimu ya kuandaa fainali za Mataifa ya Afrika 2017 (Afcon) baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuliomba Shirikisho la Soka Afrika (Caf) kuwa mwenyeji.

“Nimeona TFF wametangaza kuwa wanaomba kuandaa Afcon 2017, watu wameipokea kwa mtazamo tofauti. Hii ni nafasi ambayo hatutakiwi kuiacha, nchi yetu haijawahi kushiriki mashindano hayo tangu mwaka 1980,” alisema Zitto. Alisema: “Kuna njia mbili tu za kushiriki mashindano hayo, moja ni kufuzu na nyingine ni kuandaa fainali hizo.” 
“Kwa upande wetu tangu mwaka 1980 tumejaribu, lakini tumeshindwa hivyo njia pekee ni kuandaa ili tushiriki. Hivi mnaijua nchi inayoitwa Burkina Faso? Wao waliandaa Afcon mwaka 1998, ni nchi maskini ya kutupwa. Tunachohitaji ni kujenga viwanja tu kwa sababu hoteli nzuri tunazo,” alisema Zitto. 
Alisema kama yeye angekuwa, angeunda kamati maalumu ya kuomba zabuni hiyo ili kuhakikisha Tanzania inashinda kwa kuwa njia hiyo italinufaisha taifa kwa sababu viwanja vitakarabatiwa na pia kuandaa timu ambayo itafaa mbele ya safari.

Alisema mbali na siasa, Zitto alisema anapenda sana soka na kwamba anaipenda sana Taifa Stars hivyo anaamini kwa kuandaa Afcon itakuwa ni njia pekee ya kujitangaza kimataifa. “Timu ya taifa inapocheza popote nikiwa na nafasi huwa ninakwenda na nafanya hivyo pia ili kui-support (kuiunga mkono),” alisema Zitto. 
Kauli ya Zito imekuja siku chache baada ya TFF kujitosa kuomba kuandaa fainali hizo mwaka 2017 baada ya Libya kujitoa kutokana na sababu za kiusalama. 

Tayari TFF imeshaiandikia CAF barua kuomba uenyeji wa Afcon 2017 baada ya Kamati ya Utendaji ya TFF iliyokutana Agosti 24 mwaka huu kutoa uamuzi huo.

CHANZO: Mwananchi

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga