Wanariadha walioing’arisha Tanzania Mbio za Nyika warejea

Kocha Francis John, Joseph Panga, Bazil John, Suleiman Nyambui, Alphonce Felix, Ismail Juma wakiwa uwanja wa ndege wa Julius Nyerere.
Wanariadha watano wa timu ya taifa ya riadha wamewasili jana wakitoka kuiwakilisha  nchi katika mashindano ya dunia ya mbio za nyika yaliyofanyika mjini Guiyang, China mwanzoni mwa juma hili.

Tanzania ilishika nafasi ya sita katika nchi 51 zilizopeleka wanariadha kwenye mashindano hayo huku Ismail Juma akitua nafasi ya tisa kati ya wanariadha 111 waliokimbia kilometa 12.

Timu hiyo iliwasili uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere saa 10:55 jioni kwa Shirika la Ndege la Emirates wakiongozana na Kocha wao Francis John na kupokewa na Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha nchini (RT) Suleiman Nyambui.

Pia mwanariadha Bazil John alisema kuwa Tanzania isitegemee medali kama haiwekezi katika maandalizi kwani wamejifunza mengi walipoenda kushiriki mbio hizo.

Kocha Francis John alisema hata sasa wanariadha wamejitahidi sana kutokana na maandalizi yaliyokuwepo.

“Inatosha kusema wanastahili pongezi kwa kuing’arisha nchi katika medani ya kimataifa, tutajitahidi katika michuano mingine,” alisema Kocha Francis.

Kwa upande wake Katibu  nbMkuu wa RT, alisema baada ya wanariadha hao kurudi watawaacha kwa majuma matatu kisha wamewaandalia kambi ambayo itawaleta wanariadha 20 na makocha watatu ambao watawekwa kambini Mbulu kuanzia Aprili 28, mwaka huu kwa ajili ya mbio za majaribio za Pan African Championship  zitakazofanyika nchini Uganda Mei 31.

Itakumbukwa kwamba timu ya taifa ya Tanzania ilipeleka wanariadha watano, Fabian Nelson Sulle, John Bazil Baynit, Joseph Panga na Ismail Juma.

Comments

Popular

GIDABUDAY KUHAMASISHA UJENZI WA KIJIJI CHA MICHEZO TANZANIA LENYE JINA YA MWANARIADHA MKONGWE BW.JOHN STEPHEN AKHWARI

Rio Olympics: Brazil win men's volleyball gold, GB's Joyce takes boxing silver – as it happened

Olympics 2016: Usain Bolt completes sprint double, Jade Jones retains taekwondo title

Rio Olympics: Swimmer Lochte apologises for 'robbery' saga