RT yaburuzwa mahakamani, Mtaka atuhumu serikali
Rais wa RT aliyechaguliwa kinyume cha sheria namba 12 ya BMT iliyotungwa na bunge 1967 alinukuliwa akisema “Serikali ilikata majina ya waliokwenda nje ya nchi kujiandaa na michezo ya Jumuiya ya Madola" Laiti angejua wala asinge nena bora angepiga kimya; ‘Tangu lini serikali kwa maana ya wizara ikawa na maamuzi ya mwanariadha gani aende na yupi asiende’ RT ndiyo kiungo kati ya serikali na wachezaji. Mwanariadha chipukizi ATSON MBUGI ambaye ni mwalimu wilayani Kilindi Tanga alijikuta akisoma jina lake kwamba yupo New Zealand wakati yeye alikuwa Kilindi akifundisha darasani. Kocha maarufu nchini mwenye vigezo vya juu kabisa vya (IAAF) SAMWEL TUPA naye ameachwa kinyemela lakini jina lake likasomeka yupo New Zealand! MASWALI MAZITO : Nani aliyeenda, nani alipaswa kwenda, kwa nini majina yameleta utata, kwa nini kuna usiri? Je posho zao nani kachukua? Ni wajibu wetu kufahamu jinsi gani pesa za walipa kodi inatumika wakati kuna fungu kutoka vyama vya michezo duniani ina