Ni Jumatatu nyingine tena tunakutana wadau wa Uwanja wa Kuchonga, kama kawaida tukipeana changamoto za kispoti ili kuchochea ufanisi katika sekta hii muhimu katika jamii. Bila shaka mu wazima wa afya na mnaendelea na majukumu ya ujenzi wa taifa kama kawaida, ila kwa wale ambao hali zao si shwari kwa namna moja ama nyingine, tunawaombea nafuu ya mapema. Kama ada, kwa manufaa ya wale ambao hatukuwa nao wiki iliyopita, tupeane dondoo japo kwa ufupi kile kilichojiri Jumatatu iliyopita. Wiki iliyopita tuliangalia sakata la usajili wa aliyekuwa kiungo wa Yanga, Frank Domayo, ambaye alinyakuliwa na mabingwa wa soka Tanzania Bara, Azam FC, tukio lililowagusa mashabiki na wadau wengi wa soka hapa nchini. Lakini tulichokizungumzia, si kusajiliwa kwake Azam, bali jinsi Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), lilivyojiingiza katika suala hilo kwa mgongo wa tukio hilo kufanyika kambi ya timu ya taifa, Taifa Stars, kisha kuamua kumteua Wakili Wilson Ogunde, kwa kile kilichoitwa kuc