RAIS JAKAYA KIKWETE AMENISAIDIA KUWAPASHA VIONGOZI WA RT NA TOC;TAIFA ZIMA LINAWAOGOPA
DC asiyejali sheria za nchi 'Niliiposti habari hii 12/08/2013, JK akawapasha 19/01/2014'. Hata hivyo Rais JK bado kuna siri hajaambiwa ya kwamba viongozi wa RT walivunja sheria NO. 12 za BMT zilizotungwa na Bunge 1967. Mtaka anadai kuwa "waziri Fenella ni shemeji yake na atamlinda, Nyambui pia ni ndugu yake wa ukoo" : Wakati nchi za ulimwengu zikiwakilishwa na wanariadha wake mahiri katika mashindano ya dunia ya riadha mjini Moscow Urusi, Tanzania imevunja rekodi ya aina yake kwa viongozi wa Chama Cha Riadha Tanzania kutangulia Moscow huku wakiwaacha wanariadha nyuma. Rais wa RT (aliyechaguliwa kinyume na katiba) bila wasiwasi, aibu wala uzalendo amekwenda Moscow wiki iliyopita huku walengwa wenyewe wa mashindano ya (World Athletic Championships) ambao ni wanariadha wanaotegemewa kupeperusha bendera ya Tanzania na kupigania medali wakibaki nyuma. Cha ajabu zaidi ni pale ambapo kiongozi huyo wa RT alipofuatana na kiongozi wa zamani wa chama hic