Posts

Sports Diplomacy: Waziri Membe kupeleka wanariadha 40 nje ya nchi

Image
Mhe. Bernard Membe Tanzania inaelekea kupata nafasi ya kupeleka timu ya riadha nchini China, Ethiopia na Uturuki kwa maandalizi ya kuwanoa vijana kwa mashindano ya madola na kwa msaada wa waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe. RT imeonyesha dalili za kuchagua wanariadha mezani badala ya mashindano ya wazi ili kufanya mchujo wa kidemokrasia.  Mfumo ambao nchi za wenzetu kama Kenya wanafanya ili kuepusha upendeleo wa aina yoyote. Katibu wa RT Sulemain Nyambui amekaririwa na vyombo vya habari akidai kupeleka majina kwa waziri Membe. 'Wazalendo na wapenda haki tunadhani ipo haja ya kuandaliwa mashindano maalum yatakayopewa viwango kadha ambayo wakimbiaji wakifikia ndio wachaguliwe kwa uwazi badala ya kumpa mwanya kiongozi  moja kumpendelea ndugu ama jamaa yake' Kuna tetesi kwamba kuna vijana na makocha ambao wamehakikishiwa safari hizo kwa ahadi maalum kwamba wakijiandaa kutoa chochote watahakikishiwa wanasafiri bila kujali uwezo

Tanzania Tennis Association kuadhimisha Siku ya tenisi duniani

Image
M/ Kiti wa TTA Methusela Mbajo / katikati Jumamosi wiki hii ( March 1 st ) chama cha tenisi Tanzania (TTA) kitaungana na vyama vya tenisi duniani pamoja na wadau kusherehekea siku ya tenisi ulimwenguni. Maadhimisho hayo yatafanyika katika viwanja vya Dar Es Salaam Gymkhana Club ambapo maadhimisho yataambatana na mafunzo ya bure kwa watoto na wakubwa watakaopenda kujifunza mchezo wa tenisi. Shughuli zitaanza saa tatu asubuhi hadi saa nane mchana, mafunzo yataendeshwa na makocha waliobobea wa tenisi wakiwemo   Kiango Kipingu na Hassan Kassim . Watanzania mnakaribishwa kiingilio ni bure, ‘njoo uangalie, njoo ujifunze, njoo ufurahi’

KENYAN DOUBLE FOR KAROKI AND WACERA AT WORLD’S BEST 10K

Image
24 FEB 2014   REPORT   SAN JUAN, PUERTO RICO Kenyans Bedan Karoki and Mary Wacera made a brilliant debut on the Teodoro Moscoso bridge and prevailed over a large African contingent to become the 2014 champions at the World’s Best 10K, an   IAAF Gold Label Road Race , whose 17th edition was held Sunday (23) afternoon in the Puerto Rican capital of San Juan. For world and Olympic 10,000m finalist Karoki and 2006 world junior bronze medallist Wacera, it was their most important road win of their international career. How the races unfolded With temperatures hovering around 27°C, a large group of about 20 runners, led by New Zealander Zane Robertson, followed a pedestrian pace, covering the first three kilometres in nine minutes. The lead pack hit the half-way mark in 14:26 and was reduced to six men after eight kilometres. Karoki made his move with two kilometres to go, gaining a 50-meter lead that increased by the time he crossed the finish line in 28:35, the second-slow

KATIBA: Nyongeza ya posho yagonga mwamba

Image
Bunge la Katiba Madai ya Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba kutaka nyongeza ya posho ya vikao vya Bunge hilo yamegonga mwamba, Mwananchi limebaini.  Habari kutoka ndani ya kamati iliyoundwa na Mwenyekiti wa Muda wa Bunge la Katiba, Pandu Ameir Kificho ili kufuatilia madai hayo, zimedai kuwa baada ya uchunguzi wa kina, wajumbe wa kamati hiyo hawakuona sababu ya kupendekeza posho hizo kupandishwa. Taarifa hizo zilidai kuwa wajumbe hao wamefikia uamuzi huo baada ya kupitia viwango vya posho vinavyolipwa na  Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali na Mashirika ya Umma. Pia kamati hiyo ilichambua viwango vya posho walivyolipwa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba na viwango vya posho ya kujikimu vya Sh80, 000 kwa siku wanavyolipwa watumishi wa Serikali.  “Hili jambo linahitaji busara sana na kutazama mazingira ya nchi pia, kwa hiyo wajumbe wale baada ya kuoanisha viwango vya posho vya taasisi mbalimbali wameona Sh300,000 zinatosha,” alisema mmoja wa wajumbe ambaye

Waziri Mukangara mgeni rasmi Kilimanjaro Marathon

Image
Dr. Fenella Mukangara - Waziri Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Mhe. Dk. Fenella Mukangara anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye mbio mbio za 12 za Kilimanjaro Marathon ambazo zinatarajiwa kufanyika Jumapili ijayo tarehe 2 Machi, 2014 mjini Moshi. Aggrey Marealle, Mkurugenzi Mkuu wa Executive Solutions, waratibu wa mbio hizo alisema jana kwamba Dr. Mukangara amekubali kuwa mgeni rasmi na atahuduria sherehe ya utoaji zawadi ambapo atatoa zawadi kwa washindi kumi wa mbio defu za kilomita 42 maarufu kama Full Marathon kwa wanaume na wanawake.  “Uwepo wa waziri ni ishara ya uungaji mkono tukio hili na ameeleza kufurahishwa kwake na maandalizi ya hali ya juu ya Kilimanjaro Marathon. Dk. Mukangara ameeleza mara kadhaa kwamba serikali inaunga mkono Kilimanjaro Marathon kwa kutambua mchango wake michezo, utalii na uchumi,” alisema Marealle. Marealle aliongeza kwamba baada ya sherehe ya utoaji zawadi Waziri ataungana na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na mpenda michezo Mhe.

MATOKEO: Mfumo mpya ‘ahueni’ kidato cha nne

Image
Dr Kawambwa/Waziri Elimu   Kwa matokeo kidato cha nne 2013 bonyeza hapa: Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), limetangaza Matokeo ya Mtihani wa Taifa wa kidato cha nne wa 2013, huku ufaulu ukiongezeka kwa asilimia 15.17. Matokeo hayo ni ya kwanza tangu kuanza kutumika kwa mfumo mpya wa upangaji ambao ulipanua wigo wa alama na madaraja, hivyo kutoa nafasi kubwa zaidi kwa watahiniwa kufaulu. Licha ya kuanza kutumika kwa mfumo huo, idadi ya waliofeli imeendelea kuwa kubwa kwani watahiniwa 151,187 sawa na asilimia 42.91 wamepata sifuri. Kati ya hao, wavulana ni 78,950 sawa na asilimia 41.54 na wasichana ni 72,237 sawa na asilimia 44.51. Kadhalika matokeo hayo yameendelea kushuhudia baadhi ya watahiniwa wakiandika matusi kwenye karatasi zao za majibu, huku wengine wakichora vitu vya ajabu kwenye mitihani hiyo, huku wengine wakishindwa kuandika chochote kwenye karatasi hizo. Akitangaza matokeo hayo jana jijini Dar es Salaam, Kaimu Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde al

JK mgeni rasmi miaka 30 ya kumbukumbu ya kifo cha Sokoine

Image
Kutakuwa na mbio za kilomita 2 kwa watoto wa shule za msingi na sekondari, pia waheshimiwa viongozi wa serikali, viongozi na wakuu wa vikosi vya ulinzi na usalama pia watashiriki mbio za kilomita 2 kama ilivyokuwa mwaka jana.