Posts

Showing posts with the label Matukio

BUTIAMA: Ziara yangu nyumbani kwa baba wa taifa

Image
Safari yangu ya kuingia ndani ya boma la baba wa taifa ilianzia hapo mlangoni ambapo hisia za kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere zilinijia ghafla.   Hili jumba ndilo linalohifadhi kaburi la baba wa taifa, kimsingi ufikapo hapo utapata kujua historia kamili ya jinsi uhuru wetu ulivyopatikana. Utajifunza mengi kwa kuona mwenyewe na pia utapata kuelezwa usiyoyafahamu.   Sanamu ya baba wa taifa! Bilashaka watanzania tutajitahidi kumuenzi baba wa taifa kwa vitendo.

Miss Tanzania refutes Sitti’s age cheating claims

Image
Photo by:Texas Department of Motor Vehicle  The organizers of Miss Tanzania beauty pageant, Lino International Agency played down the allegations of age cheating facing the recent crowned Sitti Mtemvu, insisting that she is still being regarded as eventual winner unless proved otherwise. There was concern over Mtemvu’s winning of the prestigious title, alleged that she was over aged and not below 24 years as per Miss Tanzania’s participation regulations. The controversy led to the leakage of some documents, which despite showing that she was over aged, the organizers said that they do not give weight to such mere allegations unless concrete evidence is given. Speaking in Dar es Salaam yesterday, Lino International Agency managing director, Hashim Lundenga said that for that reason, Mtemvu is still the winner of 2014 Miss Tanzania and as such, still wears the crown. Lundenga said that Mtemvu’s age cheating issue has been exaggerated by rumours with no documents t

Tathmini ya Madola, ifanyiwe kazi

Image
Timu ya Tanzania kwenye michezo ya Jumuiya ya Madola yakaribishwa rasmi leo katika kijiji maalum cha michezo hiyo Glasgow Kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania, Serikali ilikutana na wanamichezo kwa ajili ya kufanya tathmini ya ushiriki wa taifa kwenye michezo ya Jumuiya ya Madola ya 2014 ambayo Tanzania ilitoka kapa kwa mara ya pili mfululizo. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ndiye alikuwa mgeni rasmi katika tathmini hiyo iliyowahusisha wachezaji, makocha na viongozi wa vyama mbalimbali vya michezo. Katika tathmini hiyo, vyama vililalamikiwa kutokuwa makini katika kuziandaa timu zao kwa ajili ya mashindano ya kimataifa. Maandalizi duni ilikuwa ni moja ya sababu kubwa iliyotajwa katika tathmini hiyo iliyohusisha wanamichezo wa ngumi, riadha, mpira wa meza, judo, kuogelea, baiskeli na kunyanyua vitu vizito walioiwakilisha nchi katika michezo ya madola iliyofanyika Scotland. Maandalizi ya zimamoto ni ugonjwa sugu ulio kw

Theresia Dismas: Mama jasiri aliyeiletea Tanzania medali ya kwanza 1965

Image
Katika medani ya kimichezo Tanzania, historia ya kuletwa medali ya kwanza katika mshindano ya kimataifa ilitekelezwa na mwanamama Theresia Dismas Watanzania hatukumjua na hata tukatabiri kwamba mama yetu Theresia Dismas hayupo duniani kama nilivyowahi kuandika katika blog hii.  Ukweli ni kwamba mtanzania wa kwanza kufungua pazia la medali yupo hai na kwamba watanzania tuanze juhudi za kumtambulisha kwa viongozi wakuu wa serikali. Nilipoandika story kuwa mwanamke ndiye aliyeleta medali wa kwanza wengi walistuka maana historia hii inayowainua wanawake ilifichwa kwa muda mrefu bila shaka kutaka kupotosha ukweli. Jana nimepigiwa simu toka Uingereza na mtoto wa Theresia Dismas akaniambia habari yote katika blog yangu ni kweli “Isipokuwa” mama yao yupo hai na salama na anaishi Kenya! 'Mimi nilistuka na kushindwa jinsi ya kumjibu ila nilifurahi kwamba blog yangu imevumbua dhahabu iliyofichwa' na kwamba nitafanya juhudi kwa kushirikiana na wazalendo wenzangu tuwez

Kwa mwenendo huu, michezo haitafanikiwa Tanzania

Image
Mama Anna Kibira / Mwenyekiti wa Chama cha Netboli Taifa(CHANETA) Kuondolewa kwa timu ya taifa ya netiboli kwenye harakati za kutafuta tiketi ya kufuzu kushiriki fainali za Kombe la Dunia ni mwendelezo wa matukio ya kusikitisha yanayoendelea kuzikumba timu za taifa za Tanzania. Chama cha Netiboli Tanzania (Chaneta) kilitangaza kuiondoa timu hiyo kutokana na kukosa fedha za gabarone, Botswana kushiriki mashindano ya Afrika ya kutafuta tiketi ya kwenda Kombe la Dunia. Huenda kwa mara ya kwanza tungeshuhudia Taifa Queens ikikata tiketi ya kushiriki michuano hiyo mikubwa, lakini ndoto hizo ziliyeyushwa na Chaneta. Chaneta ilitembeza bakuli la kutafuta fedha za kufanikisha safari hiyo, lakini haikufanikiwa. Kushindwa kwa Taifa Queens kwenda kwenye mashindano hayo ni mwendelezo wa timu za Taifa kukosa mashindano muhimu. Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) pia limekuwa likijiendesha kwa mtindo huo, hali kadhalika kwa vyama vya ngumi, kikapu, mpira wa meza, judo na

Malinzi maji ya shingo

Image
Jamal Malinzi / Rais wa Shirikisho la Mpira Tanzania (TFF) BODI ya Ligi Kuu Tanzania kwa kushirikiana na Klabu 14 za ligi hiyo, zimetishia kusaka theluthi mbili ya saini za Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ili kuitisha Mkutano Mkuu wa dharura wa kupiga kura ya kutokuwa na imani Rais wa shirikisho hilo, Jamal Malinzi. Hayo yamesemwa jana jijini Dar es Salaam na wakili wa kujitegemea Dk. Damas Ndumbaro, anayeiwakilisha TPL Board na klabu 14 za Ligi Kuu, katika jaribio lao la kupinga shinikizo la TFF kuzikata klabu hizo asilimia tano ya pesa za wadhamini wa ligi hiyo ambao ni Kampuni ya Vodacom na Azam Media Ltd. Uamuzi huo wa TPL Board na klabu za Ligi Kuu, umekuja siku moja baada ya Malinzi kusisitiza kuwa uamuzi wa kukata asilimia tano ya makato ya pesa za wadhamni kwa klabu za ligi hiyo uko palepale, na kwamba bodi hiyo haina mamlaka ya kupinga agizo hilo na wenye uwezo au mamlaka hayo ni Kamati ya Utendaji ya TFF. Akijibu hoja moja baada ya nyi

HAKI: Michezo imezingatiwa katika rasimu inayopigiwa kura?

Image
Wajumbe wa bunge maalum la katiba linaloendelea Dodoma, bunge hilo linategemewa kufikia tamati muda hivi karibuni tena huenda lisifanikishe azma na matarajio ya watanzania. Hapana wanamichezo nafasi hatukupewa japo majina yalipendekezwa kuingizwa katika lile kundi la 201.  Hata hivo wanamichezo tusichukie wala kuhuzunika maana dalili zinaonyesha wazi kwamba hakuna maridhiano yatakayoleta katiba mpya kwa sasa. Mwisho wa siku sisi “Wanamichezo” tutakuwa na thawabu sababu hatukuthubutu kujadili jambo lisilowezekana maana dalili zipo wazi. Hata hivyo tuangalie kwa macho kwanza maana kuna msemo usemao “Anayesikiliza kwa makini ndiye anayefaidi mwishoni”.  Ombi kwa wawakilishi wetu bungeni hivi sasa ‘ Tafadhali waheshimiwa msiwe mabubu katika kupigania haki za wanamichezo kama ambavyo mnapigia kelele ufujaji wa fedha za uma' 'Mkumbuke kwamba jasho la mshezaji ni gharama zaidi kuliko noti zinazochapishwa na Federal Reserves’ Ninyi kushindwa kutuwakilisha vyema

Ikangaa apigiwa debe ‘kumrithi’ Malinzi uenyekiti wa BMT

Image
Col. Rt. Juma Ikangaa Mwanariadha wa zamani , Juma Ikangaa anatajwa kurithi nafasi ya uenyekiti  wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) baada ya Dioniz Malinzi kumaliza muda wake wa miaka mitatu juzi Jumapili.  Habari za ndani ambazo gazeti hili ilizipata zilieleza kuwa kati ya majina yaliyopendekezwa na Serikali, Ikangaa anapewa nafasi kubwa ya kuchukua mikoba ya Malinzi.  “Yalipendekezwa majina kadhaa ya watu maarufu ambao Serikali iliona wanastahili kuongoza BMT baada ya Malinzi kumaliza muda wake na Ikangaa ndiye anapewa nafasi kubwa ya kuwa mwenyekiti,” kilisema chanzo chetu.  Mwenyewe (Ikangaa) alipotafutwa na gazeti hili kujua msimamo wake, hakukubali wala kukataa kutaka cheo hicho zaidi ya kueleza hana taarifa zozote juu ya uteuzi huo. Gazeti hili lilimtafuta, Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel ili k

Sugu atikisa Uwanja wa Sokoine

Image
Sugu sugu sugu… hivyo ndiyo mashabiki wa Mbeya City walivyoimba kwa muda mrefu baada ya mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ kuingia uwanjani juzi kushuhudia mechi ya Ligi Kuu kati ya Mbeya City na Coastal Union. Ilikuwa katika dakika ya 38 ya mchezo huo, wakati Sugu alipoingia uwanjani na baada ya kushuka tu kwenye gari lake, uwanja mzima ulizizima kwa kelele za mashabiki kumshangilia kwa nguvu zote  wakisema “Sugu sugu sugu”, huku wakimtaka aende kukaa kwenye eneo walilokuwapo. Sugu alilikubali wito huo na kwenda kukaa eneo la mashabiki hao. Mmoja wa viongozi waliokuwa kwenye jukwaa kuu alishuka ghafla kwa lengo la kumkaribisha Sugu meza kuu, lakini Sugu hakwenda na badala yae alinyosha njia kwenda kukaa kwa mashabiki huku akishangiliwa kwa nguvu. Akizungumza na gazeti hili, baada ya kumalizika kwa mechi hiyo, Sugu alisema hakuwa na sababu yoyote ya kukaa jukwaa kuu kwani uhondo wa mchezo ni pale unapokuwa na vijana aliowaita wenye ‘mizuka’.

Uzembe waitoa Tanzania michezo ya Olimpiki 2016

Image
Tanzania haitashiriki michezo ya soka  kimataifa hadi mwaka 2016 kutokana na timu yake ya  vijana  wa umri chini ya miaka 23  kutoshiriki michuano ya kusaka  tiketi ya kushiriki Olimpiki  msimu wa 2015/2016. Kukosekana kwa timu hiyo ya U-23 kunaweza kuwa uzembe  wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF). Katika ratiba iliyotolewa juzi na Shirikisho la Soka  Afrika (CAF), pazia la michuano hiyo litafunguliwa Desemba. Katika michuano hiyo, raundi ya kwanza  Rwanda itaanza kukata utepe kwa kumenyana na Somalia wakati Kenya itacheza na Zambia au Botswana. Kikosi hicho mara ya mwisho kilishiriki michezo ya  Afrika mwaka 2011,  kikiwa chini ya Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ na kiliondolewa mapema kwenye michuano hiyo na Nigeria.  Hata hivyo, U-23 haitashiriki michuano hiyo kwa vile Tanzania haikuthibitisha ushiriki wake huku viongozi wa juu wa TFF wakikwepa kulizungumzia  suala hilo.

Bodi ya ngumi iundwe kunusuru mabondia

Image
Rais wa TPBO Yassin Abdallah 'Ustadhi' akikabidhi vyeti Mchezo wa ngumi za kulipwa ni miongoni mwa michezo inayoongoza kwa kupendwa hapa nchini, tukiachilia mbali soka ambao unaongoza kupendwa zaidi. Licha ya mchezo wa ngumi za kulipwa kuwa na nafasi kubwa kwa mashabiki kinachosikitisha ni namna mabondia wa ngumi za kulipwa hapa nchini wanavyotumika kuwaneemesha wengine huku wao wakiambulia fedha ya madafu na wakati mwingine kudhulumiwa kabisa. Kumekuwa na matukio mengi ya mabondia kudhulumiwa ambayo nikianza kuyaorodhesha huenda ukurasa huu ukajaa na usitoshe, kwani imekuwa ni kawaida viongozi wa ngumi za kulipwa kuwatumia kama madaraja mabondia. Hiyo yote inachangiwa na mfumo wa uongozi wa ngumi za kulipwa tulionao hapa nchini, japo tunaambiwa ngumi za kulipwa ni biashara, lakini ubabaishaji umekithiri kwa viongozi wake kuendesha mchezo huo wanavyotaka wao. Huu utaratibu wa ngumi za kulipwa kusimamiwa na kampuni za TPBO Limited chini ya rais wake, Yassin Abdall

Archive: The Arusha manifesto by Mwl Julius Nyerere

Image

Hatimaye RT wakabwa mahakamani kwa madai ya Milioni 20

Image
Suleiman Nyambui / Katibu mkuu wa Chama Cha Riadha Tanzania Kampuni ya SYMAITON SAPALI & CATHY CATERING imewaburuza viongozi wa Chama Cha Riadha Tanzania RT kwa deni la Tsh: 20,000,000 iliyotokana na chakula cha wanariadha wakati wa mashindano ya taifa yaliyofanyika Dar Es Salaam September 2012. Kesi hiyo (Civil Case Number 9/2014) ilifunguliwa katika mahakama ya wilaya ya Temeke siku za nyuma huku viongozi wa RT wakikaidi wito wa mahakama. Juzi (September 11, 2014) Katibu wa RT Suleiman Nyambui alihudhuria kesi hiyo baada ya mahakama kutoa amri kali ambapo angedharau amri hiyo huenda angekamatwa na kutiwa ndani. Akihojiwa na kituo kimoja cha redio hapo jana, Nyambui alikana kesi hiyo yenye kutia doa chama cha riadha, lakini muda mfupi baadae mwanasheria wa RT Thabit Bashir alithibitisha kuwepo kwa kesi hiyo. Hivi karibuni Suleiman Nyambui amekuwa akiandamwa kote kote hadi kutiliwa shaka katika biashara ya madawa ya kulevya!  Akisthibitisha yeye mw

Trouble looms for TTA officials

Image
Fina Mango/TTA Vice President The National Sports Council (NSC) has given Tanzania Tennis Association (TTA) a seven-day ultimatum to provide details as to why the body has not reported to meetings which the council has been holding to solve wrangles in the association.   NSC officer Benson Chacha who is responsible for tennis desk confirmed that NSC has dispatched a letter to TTA leadership on the matter.   He said NSC has on four occasions invited TTA for meetings but neither showed up, nor gave any excuse.   ‘On Wednesday the Chairman of NSC was there waiting for them but they never showed up, so we have decided to write them to explain as to why they are failing to attend the meetings. NSC rules are clear on disciplinary action which can be taken on such cases, but we want the officials to explain and also defend themselves,’ he said.   According to Chacha, early this year some members of TTA complained to NSC on the way the association is run, the me

Zitto azitaka fainali za Afrika 2017

Image
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ameishauri Serikali isiache nafasi adimu ya kuandaa fainali za Mataifa ya Afrika 2017 (Afcon) baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuliomba Shirikisho la Soka Afrika (Caf) kuwa mwenyeji. “Nimeona TFF wametangaza kuwa wanaomba kuandaa Afcon 2017, watu wameipokea kwa mtazamo tofauti. Hii ni nafasi ambayo hatutakiwi kuiacha, nchi yetu haijawahi kushiriki mashindano hayo tangu mwaka 1980,” alisema Zitto. Alisema: “Kuna njia mbili tu za kushiriki mashindano hayo, moja ni kufuzu na nyingine ni kuandaa fainali hizo.”  “Kwa upande wetu tangu mwaka 1980 tumejaribu, lakini tumeshindwa hivyo njia pekee ni kuandaa ili tushiriki. Hivi mnaijua nchi inayoitwa Burkina Faso? Wao waliandaa Afcon mwaka 1998, ni nchi maskini ya kutupwa. Tunachohitaji ni kujenga viwanja tu kwa sababu hoteli nzuri tunazo,” alisema Zitto.  Alisema kama yeye angekuwa, angeunda kamati maalumu ya kuomba zabuni hiyo ili kuhakikisha Tanzania inashinda kwa kuwa n

Nyambui ataka kung’atuka RT

Image
Katibu wa Chama cha Riadha Tanzania (RT), Suleiman Nyambui amemtaka mtu yeyote anayeweza kuongoza chama hicho ajitokeze ili yeye ang’atuke na kumwachia madaraka. Nyambui alisema katika mahojiano kuwa yuko tayari kujiuzulu wadhifa huo ndani ya RT kama atatokea mtu ambaye anadhani akimwachia cheo hicho ataweza kuleta mafanikio katika mchezo huo. Kigogo huyo wa RT alisema amekuwa akifanyiwa fitina na baadhi ya watu waliowahi kumshawishi kuungana nao ili wapate fursa ya kuitumia RT kufanya maovu yao, lakini walipokumbana na ‘kigingi’ chake wameanza kumfanyia fitina. “Baadhi ya watu wananizungumzia vibaya. Lakini niko tayari kuondoka RT hata leo kama mimi ndiyo kikwazo cha mafanikio ya riadha endapo tu akitokea mtu ambaye atanithibitishia kuwa ana uwezo wa kuleta mafanikio,” alisema Nyambui. CHANZO: Mwananchi

Tufanye sensa ya vyama vya michezo nchini

Image
Dioniz Malinzi / Bosi wa Baraza la Michezo Tanzania Mwaka 2014 unakaribia kumalizika. Ni dhahiri hali ni mbaya katika medani ya michezo nchini na hiyo ni kutokana na matokeo tuliyoona kwa timu na wanamichezo wetu. Kimsingi, Tanzania imeharibu na kutia aibu kuanzia soka, ambayo ndiyo mchezo maarufu, hadi michezo mingine. Viongozi wenye dhamana katika michezo na wao wanaingiza siasa badala ya kuangalia nini wajibu wao na kwa chama na manufaa ya taifa. Tumewahi kupiga kelele sana katika eneo la michezo kuwa udhaifu wa uongozi na hasa kwa kutokuwa na dhamira na dira ya maendeleo, ndiyo kunachangia kutopiga hatua. Kuvurunda kwa wanamichezo wa Tanzania katika mashindano mbalimbali, kutokana na kukosa umakini na zaidi ni udhaifu wa uongozi katika vyama na klabu. Kwa jinsi hiyo, itachukua muda mrefu Tanzania kupiga hatua katika michezo kama mfumo wa utendaji ndani ya vyama hautabadilika. Kutokana na msingi huo, kuna haja kwa mamlaka inayohusika na michezo yote kufany

Okwi arejea Simba

Image
Emmanuel Okwi /Mchezaji maarufu wa soka HATIMAYE mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda, Emmanuel Okwi, jana amesaini kuichezea klabu yake ya zamani ya Simba kwa mkataba wa miaka miwili. Habari zilizopatikana jana jioni, zilisema nyota huyo ambaye hatima yake ndani ya klabu ya Yanga ilikuwa gumzo kubwa, jana alitarajiwa kusaini mkakaba huo kuwatumikia Wekundu wa Msimbazi kwa kipindi kingine. Kurejea kwa Okwi Msimbazi, kunamweka katika wakati mgumu mchezaji Benard Musoti, nyota wa kimataifa wa Kenya, kwani sasa ni yeye sasa anayechungulia dirisha la kutokea, ama Pierre Kwizera. Okwi kutua Simba, ni kama kurejea nyumbani kwani ndio klabu aliyojiunga nayo kwa mara ya kwanza nchini akitokea Uganda na kung’ara nayo, kabla ya kuihama na kujiunga Etoile du Sahel ya Tunisia na kisha Yanga. Sheria za usajili za Ligi Kuu Tanzania Bara zinataka klabu kuwa na nyota wa kigeni wasiozidi watano na mbali ya Okwi, nyota wengine wa kimataifa katika kikosi cha Simba ni, Raphael Kiongera, Joseph O

Michezo: Tufanye yafuatayo ili tusonge mbele

Image
Bernard Membe/Waziri mambo ya Nje Viongozi wa vyama vya michezo wanapaswa kurejesha serikalini ripoti ya jinsi maandalizi, safari na mashindano yalivyofanyika wakati wa mashindano ya Glasgow. Itakuwa ni kosa kubwa iwapo vyama vya michezo vitakabidhi ripoti zao kwa mkurugenzi wa michezo, badala yake viongozi wa vyama wakabidhi wenyewe. Pia itakuwa ni haki kabisa wataalamu wa michezo husika kushirikishwa siku ya ripoti hiyo kuwasilishwa ili nao watoe ushauri wao wa kitaalamu. Wachezaji walioshiriki pia wahusishwe ili waweze kusema yao ya mioyoni kwa uhuru na uwazi. ‘Hayo yakifanyika tutafanya vizuri safari ijayo kwani tutakuwa tumejua wapi tulijikwaa’